Friday, 16 February 2018

TAMBUA KUSUDI LA WEWE KUWEPO HAPA DUNIANI

TAMBUA KUSUDI LA WEWE KUWEPO HAPA DUNIANI

"Janga kubwa katika maisha sio kifo bali ni maisha bila kusudi"    
       Dr. Myles Munroe


Msingi unatoka katika kitabu cha Yohana 15 : 16

 Si ninyi mlionichagua mimi, bali ni mimi niliyewachagua ninyi; nami nikawaweka mwende mkazae matunda; na matunda yenu yapate kukaa; ili kwamba lo lote mmwombalo Baba kwa jina langu awapeni.

Twende taratibu sasa....


JAMBO LA KWANZA

 Si ninyi mlionichagua mimi, bali ni mimi niliyewachagua ninyi;

Haya ni maneno ya Yesu ukianza kusoma mistari ya nyuma utaona alikuwa katika kufundisha...

Yesu ndiye Mungu ambaye ndiye roho mtakatifu Utatu ndani ya Mungu mmoja...

Huyu ndiye aliyetuweka hapa duniani ndiye aliyesema katika

Mwanzo 1
27 - Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba.


NOTE
Tambua kuwa yupo haujajiweka hapa duniani.. aliyekuweka na ndiye mwenye sababu ya wewe kuishi hapa duniani



 JAMBO LA PILI

.nami nikawaweka mwende mkazae matunda;

Baada ya kuwa tumechaguliwa au kuumbwa kwa mfano wa Mungu na kujua kwa nini tumeumbwa tunapaawa kuzaa..

hapa haimaanishi kujifungua...😂😂

 Anamaanisha vile tulivyonavyo tuviongeze/ tuvikuze/ tuvilee au tuviboreshe na tuwafundishe wengine kuvifanya nao wafanye ili kujenga Ufalme wa Mungu

Tazama Mwanzo 1 : 28
"Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi,"

tunapaswa kuanza kutafuta ni jambo gani unaloweza kulifanya kwa urahisi linalompa Mungu utukufu na litakalowaleta watu kwa Yesu, hususan kwa karama uliyo nayo. Hapo tutakuwa tunazaa matunda.

NOTE
Tambua karama/vipawa na uwezo ulionao unapaswa utumike kushare na wengine na kuwaleta wengine kwa Yesu...huko ndiko kuzaa matunda



JAMBO LA TATU

 matunda yenu yapate kukaa;

Hapa linazungumziwa suala la uendelevu yale matunda tunayoyazaa tusiyapoteze tuhakikishe yanaendelea kuwepo siku zote tena nayo yazae matunda mengine mengi...

Hatupaswi kuchoka katika kuyatunza yale matunda yetu mema ili yaendelee kukaa nayo yazae..

Wagalatia 6 : 9

 "Tena tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho."

 NOTE
Tambua unapozaa matunda yako hakikisha huchoki kuyatunza yaani kuyafanya yakae kwenye haki ile ile ya ufresh



JAMBO LA NNE

ili kwamba lo lote mmwombalo Baba kwa jina langu awapeni.

Hapa kuna suprise hapa mmeiona?

 kumbe yoote hayo tuliyokuwa tunayafanya hapo juu yana jambo jema hapa mwisho

Kumbe tukifanya...

1. Kuzaa matunda.

2. Kuyafanya yadumu.

3.Halafu tukimuomuomba Mungu kwa Jina La Yesu tunapewa

Hakuna shida wala matatizo tena ikiwa tutafuata kanuni hii aliyoiweka muumbaji wetu. ndio maana neno anasema katika..

Mathayo 6:33

"Utafuteni kwanza ufalme wake na haki yake na hayo mengine mtazidishiwa."


NOTE

1. Kumzalia Mungu matunda na Kuyafanya yakae ndio kusudi la Mungu kutuumba.

2. Ndipo penye majibu ya mahitaji yetu yotee


Basi kwa neno hili tuhitimishe hivi...

Kwa wale tunaohangaika na kutumia nguvu sana kuomba hatupati majibu inawezekana hatujafuata utaratibu/kanuni...
  
jaribu kuishi kwa utaratibu huu utapata majibu haraka.

1. Zaa matunda
2. Yafanye yakae

 Baada ya hayo omba lolote sasa.

Mbarikiwe sana.


Dr James  Makala
0763 832798


©truth about success

Wednesday, 7 February 2018

CHAKULA CHAKO NI DAWA.

“KIFANYE CHAKULA KIWE DAWA YAKO NA DAWA YAKO IWE CHAKULA”
By Hippokrates 460KK-370KK Larisa - Ugiriki


Huu ni msemo uliosemwa na mtaalamu wa kiwango cha juu kabisa katika kada ya utabibu (udaktari) na alijulikana kama baba wa uganga (father of medicine) na hata leo waganga hufuata kiapo kinachosemakana kilitungwa na Hippokrates. Anafahamika kwa mtindo wake wa kuangalia magonjwa uliokuwa ni mpya wakati ule.

Hakuamini tena kuwa ugonjwa unasababishwa na mapepo au uchawi na kurogwa, alichunguza na kugundua kuwa magonjwa mengi yanasababishwa na matatizo ndani ya mwili. Ndipo baadae alipokuja na msemo wake huo hapo juu kwamba
  

“kifanye chakula kiwe dawa yako na dawa yako iwe chakula”


                    Picha ya Hippokrates (baba wa uganga)

Kimsingi chakula tunachokula kinasababisha matokeo makubwa sana katika afya zetu pamoja na uwezo miili yetu kuendelea kuishi, haijalishi kama unajua hili ama haujui matokeo ya kile unachokula yatatokea tu. Kuwa na ufahamu zaidi juu ya masuala ya mlo na sifa za uponyaji utokanao na vyakula, utakusaidia kufanya mabadiliko katika suala zima la ulaji ili uweze kufikia mahitaji ya mwili wako. Na hii itakusaidia kwa kiwango kikubwa kuimarisha na kuboresha afya yako.


NGUVU YA ULINZI KATIKA CHAKULA.

Sayansi mlo (nutritional science) imeangazia zaidi katika umuhim wa chakula kisichotengenezwa viwandani (whole food) :

kutoka hapo tunaelewa kuwa virutubisho vilivyomo ndani ya chakula vinafanya kazi kwa ushirikiano ili kuboresha afya zetu— ambapo vyakula vya kusindikwa (processed food) vinapoteza kiasi kikubwa cha virutubisho, na vinaweza kusababisha magonjwa.

Tujue kuwa vitamin, amino asidi, madini, na mafuta ya muhimu takribani 50 kwa idadi au zaidi zinahitajika katika kila mlo tunaoupata. Na zaidi ya virutubisho-mimea (phyto-nutrients) 1200 vinapatikana katika matunda, mbogamboga, mbegu na vyakula vitokanavyo na wanyama.


Itaendelea….

Dr. James Makala.
0763 832798

© truth about success

Thursday, 1 February 2018

People generally fall into one of three groups:

 the few who make things happen,

the many who watch things happen, and

the over-whelming majority who have no notion of what happens.

*Myles Munroe*