Friday, 16 February 2018

TAMBUA KUSUDI LA WEWE KUWEPO HAPA DUNIANI

TAMBUA KUSUDI LA WEWE KUWEPO HAPA DUNIANI

"Janga kubwa katika maisha sio kifo bali ni maisha bila kusudi"    
       Dr. Myles Munroe


Msingi unatoka katika kitabu cha Yohana 15 : 16

 Si ninyi mlionichagua mimi, bali ni mimi niliyewachagua ninyi; nami nikawaweka mwende mkazae matunda; na matunda yenu yapate kukaa; ili kwamba lo lote mmwombalo Baba kwa jina langu awapeni.

Twende taratibu sasa....


JAMBO LA KWANZA

 Si ninyi mlionichagua mimi, bali ni mimi niliyewachagua ninyi;

Haya ni maneno ya Yesu ukianza kusoma mistari ya nyuma utaona alikuwa katika kufundisha...

Yesu ndiye Mungu ambaye ndiye roho mtakatifu Utatu ndani ya Mungu mmoja...

Huyu ndiye aliyetuweka hapa duniani ndiye aliyesema katika

Mwanzo 1
27 - Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba.


NOTE
Tambua kuwa yupo haujajiweka hapa duniani.. aliyekuweka na ndiye mwenye sababu ya wewe kuishi hapa duniani



 JAMBO LA PILI

.nami nikawaweka mwende mkazae matunda;

Baada ya kuwa tumechaguliwa au kuumbwa kwa mfano wa Mungu na kujua kwa nini tumeumbwa tunapaawa kuzaa..

hapa haimaanishi kujifungua...😂😂

 Anamaanisha vile tulivyonavyo tuviongeze/ tuvikuze/ tuvilee au tuviboreshe na tuwafundishe wengine kuvifanya nao wafanye ili kujenga Ufalme wa Mungu

Tazama Mwanzo 1 : 28
"Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi,"

tunapaswa kuanza kutafuta ni jambo gani unaloweza kulifanya kwa urahisi linalompa Mungu utukufu na litakalowaleta watu kwa Yesu, hususan kwa karama uliyo nayo. Hapo tutakuwa tunazaa matunda.

NOTE
Tambua karama/vipawa na uwezo ulionao unapaswa utumike kushare na wengine na kuwaleta wengine kwa Yesu...huko ndiko kuzaa matunda



JAMBO LA TATU

 matunda yenu yapate kukaa;

Hapa linazungumziwa suala la uendelevu yale matunda tunayoyazaa tusiyapoteze tuhakikishe yanaendelea kuwepo siku zote tena nayo yazae matunda mengine mengi...

Hatupaswi kuchoka katika kuyatunza yale matunda yetu mema ili yaendelee kukaa nayo yazae..

Wagalatia 6 : 9

 "Tena tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho."

 NOTE
Tambua unapozaa matunda yako hakikisha huchoki kuyatunza yaani kuyafanya yakae kwenye haki ile ile ya ufresh



JAMBO LA NNE

ili kwamba lo lote mmwombalo Baba kwa jina langu awapeni.

Hapa kuna suprise hapa mmeiona?

 kumbe yoote hayo tuliyokuwa tunayafanya hapo juu yana jambo jema hapa mwisho

Kumbe tukifanya...

1. Kuzaa matunda.

2. Kuyafanya yadumu.

3.Halafu tukimuomuomba Mungu kwa Jina La Yesu tunapewa

Hakuna shida wala matatizo tena ikiwa tutafuata kanuni hii aliyoiweka muumbaji wetu. ndio maana neno anasema katika..

Mathayo 6:33

"Utafuteni kwanza ufalme wake na haki yake na hayo mengine mtazidishiwa."


NOTE

1. Kumzalia Mungu matunda na Kuyafanya yakae ndio kusudi la Mungu kutuumba.

2. Ndipo penye majibu ya mahitaji yetu yotee


Basi kwa neno hili tuhitimishe hivi...

Kwa wale tunaohangaika na kutumia nguvu sana kuomba hatupati majibu inawezekana hatujafuata utaratibu/kanuni...
  
jaribu kuishi kwa utaratibu huu utapata majibu haraka.

1. Zaa matunda
2. Yafanye yakae

 Baada ya hayo omba lolote sasa.

Mbarikiwe sana.


Dr James  Makala
0763 832798


©truth about success

No comments:

Post a Comment