“KIFANYE
CHAKULA KIWE DAWA YAKO NA DAWA YAKO IWE CHAKULA”
By Hippokrates
460KK-370KK Larisa - Ugiriki
Huu ni msemo uliosemwa na
mtaalamu wa kiwango cha juu kabisa katika kada ya utabibu (udaktari) na
alijulikana kama baba wa uganga (father of medicine) na hata leo waganga
hufuata kiapo kinachosemakana kilitungwa na Hippokrates. Anafahamika kwa mtindo
wake wa kuangalia magonjwa uliokuwa ni mpya wakati ule.
Hakuamini tena kuwa ugonjwa
unasababishwa na mapepo au uchawi na kurogwa, alichunguza na kugundua kuwa
magonjwa mengi yanasababishwa na matatizo ndani ya mwili. Ndipo baadae
alipokuja na msemo wake huo hapo juu kwamba
“kifanye
chakula kiwe dawa yako na dawa yako iwe chakula”
Picha
ya Hippokrates (baba wa uganga)
Kimsingi chakula tunachokula kinasababisha
matokeo makubwa sana katika afya zetu pamoja na uwezo miili yetu kuendelea
kuishi, haijalishi kama unajua hili ama haujui matokeo ya kile unachokula
yatatokea tu. Kuwa na ufahamu zaidi juu ya masuala ya mlo na sifa za uponyaji
utokanao na vyakula, utakusaidia kufanya mabadiliko katika suala zima la ulaji
ili uweze kufikia mahitaji ya mwili wako. Na hii itakusaidia kwa kiwango
kikubwa kuimarisha na kuboresha afya yako.
NGUVU YA ULINZI KATIKA
CHAKULA.
Sayansi mlo (nutritional science) imeangazia zaidi katika umuhim wa chakula kisichotengenezwa viwandani (whole food) :
kutoka hapo tunaelewa kuwa
virutubisho vilivyomo ndani ya chakula vinafanya kazi kwa ushirikiano ili
kuboresha afya zetu— ambapo vyakula vya kusindikwa (processed food) vinapoteza
kiasi kikubwa cha virutubisho, na vinaweza kusababisha magonjwa.
Tujue kuwa vitamin, amino
asidi, madini, na mafuta ya muhimu takribani 50 kwa idadi au zaidi zinahitajika
katika kila mlo tunaoupata. Na zaidi ya virutubisho-mimea
(phyto-nutrients) 1200 vinapatikana katika matunda, mbogamboga, mbegu na
vyakula vitokanavyo na wanyama.
Itaendelea….
No comments:
Post a Comment