. (A man from Genesis 2:15,16&18)
1. A Man who is in God's presence (not only saved/born again)
2. A Man who is working (earning something for his life).
3. A Man who can cultivate you, Grow somethings out of you, Develop your abilities etc
4. A Man how can protect you. Out of every threat that comes arround you.
5. A man who keep and Live the word of God.
Thursday, 25 October 2018
Wednesday, 25 April 2018
Sunday, 4 March 2018
TYPHOID FEVER/homa ya matumbo
TYPHOID FEVER/homa ya matumbo
Habari za leo ndugu msomaji wa blog ya KUSUDI LAKO. Karibuni katika somo la leo ambapo tunazungumzia ugonjwa wa homa ya tumbo ambao kwa lugha ya kitaalamu unaitwa Typhoid umezoeleka kwa jina la TAIFODI
UTANGULIZI
Typhoid ni nini?
Typhoid au Enteric fever au Homa ya matumbo ni ugonjwa wa tumbo unaoenezwa na Bacteria/vimelea waitwao Salmonella Typhi (Typhi ndipo jina Typhoid limepatikana)
MAAMBUKIZI
Kama nilivyo eleza awali katika utangulizi, Typhoid au homa ya matumbo ni ugonjwa unaosababishwa na Bacteria aitwae Salmonella Typhi.
Bacteria ni vimelea au viumbe wadogo sana wanaoweza kusababisha magonjwa na mfano wa magonjwa yanayoenezwa na Bacteria ni Tonsilitis/matezi,Urinary tract infection/UTI,Pneumonia au homa ya mapafu.Otitis media/maskio kutoa usaha..... nakadhalika.
Salmonella mdudu anaesababisha Typhoid hupatikana hasa mazingira yenye bakteria hawa na mara nyingi watu huupata kupitia maji yasiochemshwa na yenye vimelea wa Salmonella. pia hali ya matumizi mabaya ya vyoo na usafi duni (poor sanitation), hivyo basi jihadhari na ulaji wa Vitu kama kachumbari usizojua utengenezaji wake, pia jitahidi kuosha matunda kwa maji yaliochemshwa, kukausha vyombo vya kulia, kufuta mikono au kukausha baada ya kunawa wakati wa kula, kunywa maji yaliochemshwa au kutibiwa isipokua ya mvua
DALILI
1.Homa/fever hali ya mwili kupata joto
2.Body malaise-mwili kuchoka na kukosa nguvu
3.Abdominal pain-tumbo kuuma au kuunguruma na wakati mwingine kuharisha
Hii pia huweza kusababisha kuhara damu kama haitatibika mapema sababu wadudu hutoboa utumbo(intestinal perforation)
4.Headche-kuumwa kichwa
nakadhalika
5.Joints Pain/kuumwa viungo vya mwili
6.Nausea and vomiting sometimes/kichefuchefu na kutapika wakati mwingine(SIO LAZIMA)
VIPIMO
Typhoid hupimwa kwa kipimo kinaitwa Widal test under titration method ambacho huelezea kiwango cha wadudu katika damu
Mfano STH 1:80, STO 1:320
TIBA
Typhoid hutibika vizuri japo tiba haikupi kinga na unaweza ugua tena kama hutozingatia kanuni za Afya
Mfano wa dawa ambazo hutibu ni
Ciprofloxacin
Norfloxacin
Levofloxacin
Cefalexin
Ceftriaxone
Amoxycilline na kadhalika
USHAURI
Usinunue dawa na kumeza bila kupima ama ushauri wa daktari kwani wataalamu na vipimo ndivyo vinaweza kutofautisha homa na magonjwa tofauti tofauti.
AHSANTENI NA KARIBUNI KWA MASWALI.
DR. James
0763 832798
jamesmakala40@gmail.com
Truth about success
Habari za leo ndugu msomaji wa blog ya KUSUDI LAKO. Karibuni katika somo la leo ambapo tunazungumzia ugonjwa wa homa ya tumbo ambao kwa lugha ya kitaalamu unaitwa Typhoid umezoeleka kwa jina la TAIFODI
UTANGULIZI
Typhoid ni nini?
Typhoid au Enteric fever au Homa ya matumbo ni ugonjwa wa tumbo unaoenezwa na Bacteria/vimelea waitwao Salmonella Typhi (Typhi ndipo jina Typhoid limepatikana)
MAAMBUKIZI
Kama nilivyo eleza awali katika utangulizi, Typhoid au homa ya matumbo ni ugonjwa unaosababishwa na Bacteria aitwae Salmonella Typhi.
Bacteria ni vimelea au viumbe wadogo sana wanaoweza kusababisha magonjwa na mfano wa magonjwa yanayoenezwa na Bacteria ni Tonsilitis/matezi,Urinary tract infection/UTI,Pneumonia au homa ya mapafu.Otitis media/maskio kutoa usaha..... nakadhalika.
Salmonella mdudu anaesababisha Typhoid hupatikana hasa mazingira yenye bakteria hawa na mara nyingi watu huupata kupitia maji yasiochemshwa na yenye vimelea wa Salmonella. pia hali ya matumizi mabaya ya vyoo na usafi duni (poor sanitation), hivyo basi jihadhari na ulaji wa Vitu kama kachumbari usizojua utengenezaji wake, pia jitahidi kuosha matunda kwa maji yaliochemshwa, kukausha vyombo vya kulia, kufuta mikono au kukausha baada ya kunawa wakati wa kula, kunywa maji yaliochemshwa au kutibiwa isipokua ya mvua
DALILI
1.Homa/fever hali ya mwili kupata joto
2.Body malaise-mwili kuchoka na kukosa nguvu
3.Abdominal pain-tumbo kuuma au kuunguruma na wakati mwingine kuharisha
Hii pia huweza kusababisha kuhara damu kama haitatibika mapema sababu wadudu hutoboa utumbo(intestinal perforation)
4.Headche-kuumwa kichwa
nakadhalika
5.Joints Pain/kuumwa viungo vya mwili
6.Nausea and vomiting sometimes/kichefuchefu na kutapika wakati mwingine(SIO LAZIMA)
VIPIMO
Typhoid hupimwa kwa kipimo kinaitwa Widal test under titration method ambacho huelezea kiwango cha wadudu katika damu
Mfano STH 1:80, STO 1:320
TIBA
Typhoid hutibika vizuri japo tiba haikupi kinga na unaweza ugua tena kama hutozingatia kanuni za Afya
Mfano wa dawa ambazo hutibu ni
Ciprofloxacin
Norfloxacin
Levofloxacin
Cefalexin
Ceftriaxone
Amoxycilline na kadhalika
USHAURI
Usinunue dawa na kumeza bila kupima ama ushauri wa daktari kwani wataalamu na vipimo ndivyo vinaweza kutofautisha homa na magonjwa tofauti tofauti.
AHSANTENI NA KARIBUNI KWA MASWALI.
DR. James
0763 832798
jamesmakala40@gmail.com
Truth about success
Tuesday, 20 February 2018
Friday, 16 February 2018
TAMBUA KUSUDI LA WEWE KUWEPO HAPA DUNIANI
TAMBUA KUSUDI LA WEWE
KUWEPO HAPA DUNIANI
"Janga kubwa katika
maisha sio kifo bali ni maisha bila kusudi"
Dr. Myles Munroe
Msingi unatoka katika
kitabu cha Yohana 15 : 16
Si ninyi mlionichagua
mimi, bali ni mimi niliyewachagua ninyi; nami nikawaweka mwende mkazae matunda;
na matunda yenu yapate kukaa; ili kwamba lo lote mmwombalo Baba kwa jina langu
awapeni.
Twende taratibu sasa....
JAMBO LA KWANZA
Si ninyi mlionichagua mimi, bali ni mimi
niliyewachagua ninyi;
Haya ni maneno ya Yesu ukianza kusoma mistari ya nyuma
utaona alikuwa katika kufundisha...
Yesu ndiye Mungu ambaye ndiye roho mtakatifu Utatu ndani ya
Mungu mmoja...
Huyu ndiye aliyetuweka hapa duniani ndiye aliyesema katika
Mwanzo 1
27 - Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu
alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba.
NOTE
Tambua kuwa yupo haujajiweka hapa duniani.. aliyekuweka na
ndiye mwenye sababu ya wewe kuishi hapa duniani
JAMBO LA PILI
.nami nikawaweka
mwende mkazae matunda;
Baada ya kuwa
tumechaguliwa au kuumbwa kwa mfano wa Mungu na kujua kwa nini tumeumbwa
tunapaawa kuzaa..
hapa haimaanishi kujifungua...😂😂
Anamaanisha vile
tulivyonavyo tuviongeze/ tuvikuze/ tuvilee au tuviboreshe na tuwafundishe
wengine kuvifanya nao wafanye ili kujenga Ufalme wa Mungu
Tazama Mwanzo 1 : 28
"Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke,
mkaijaze nchi,"
tunapaswa kuanza
kutafuta ni jambo gani unaloweza kulifanya kwa urahisi linalompa Mungu utukufu
na litakalowaleta watu kwa Yesu, hususan kwa karama uliyo nayo. Hapo tutakuwa tunazaa matunda.
NOTE
Tambua karama/vipawa na uwezo ulionao unapaswa utumike
kushare na wengine na kuwaleta wengine kwa Yesu...huko ndiko kuzaa matunda
JAMBO LA TATU
matunda yenu yapate kukaa;
Hapa linazungumziwa suala la uendelevu yale matunda
tunayoyazaa tusiyapoteze tuhakikishe yanaendelea kuwepo siku zote tena nayo
yazae matunda mengine mengi...
Hatupaswi kuchoka katika kuyatunza yale matunda yetu mema
ili yaendelee kukaa nayo yazae..
Wagalatia 6 : 9
"Tena tusichoke katika
kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho."
NOTE
Tambua unapozaa matunda yako hakikisha huchoki kuyatunza
yaani kuyafanya yakae kwenye haki ile ile ya ufresh
JAMBO LA NNE
ili kwamba lo lote
mmwombalo Baba kwa jina langu awapeni.
Hapa
kuna suprise hapa mmeiona?
kumbe yoote hayo tuliyokuwa
tunayafanya hapo juu yana jambo jema hapa mwisho
Kumbe tukifanya...
1. Kuzaa matunda.
2. Kuyafanya yadumu.
3.Halafu tukimuomuomba Mungu kwa Jina La Yesu tunapewa
Hakuna shida wala matatizo tena ikiwa tutafuata kanuni hii aliyoiweka muumbaji wetu. ndio maana neno anasema katika..
Mathayo 6:33
"Utafuteni kwanza ufalme wake na haki yake na hayo mengine
mtazidishiwa."
NOTE
1. Kumzalia Mungu matunda na Kuyafanya yakae ndio kusudi la
Mungu kutuumba.
2. Ndipo penye majibu ya mahitaji yetu yotee
Basi kwa neno hili tuhitimishe hivi...
Kwa wale tunaohangaika na kutumia nguvu sana kuomba hatupati majibu
inawezekana hatujafuata utaratibu/kanuni...
jaribu kuishi kwa utaratibu
huu utapata majibu haraka.
1. Zaa matunda
2. Yafanye yakae
Baada ya hayo omba lolote
sasa.
Mbarikiwe sana.
Dr James Makala
0763 832798
©truth about success
Wednesday, 7 February 2018
CHAKULA CHAKO NI DAWA.
“KIFANYE
CHAKULA KIWE DAWA YAKO NA DAWA YAKO IWE CHAKULA”
By Hippokrates
460KK-370KK Larisa - Ugiriki
Huu ni msemo uliosemwa na
mtaalamu wa kiwango cha juu kabisa katika kada ya utabibu (udaktari) na
alijulikana kama baba wa uganga (father of medicine) na hata leo waganga
hufuata kiapo kinachosemakana kilitungwa na Hippokrates. Anafahamika kwa mtindo
wake wa kuangalia magonjwa uliokuwa ni mpya wakati ule.
Hakuamini tena kuwa ugonjwa
unasababishwa na mapepo au uchawi na kurogwa, alichunguza na kugundua kuwa
magonjwa mengi yanasababishwa na matatizo ndani ya mwili. Ndipo baadae
alipokuja na msemo wake huo hapo juu kwamba
“kifanye
chakula kiwe dawa yako na dawa yako iwe chakula”
Picha
ya Hippokrates (baba wa uganga)
Kimsingi chakula tunachokula kinasababisha
matokeo makubwa sana katika afya zetu pamoja na uwezo miili yetu kuendelea
kuishi, haijalishi kama unajua hili ama haujui matokeo ya kile unachokula
yatatokea tu. Kuwa na ufahamu zaidi juu ya masuala ya mlo na sifa za uponyaji
utokanao na vyakula, utakusaidia kufanya mabadiliko katika suala zima la ulaji
ili uweze kufikia mahitaji ya mwili wako. Na hii itakusaidia kwa kiwango
kikubwa kuimarisha na kuboresha afya yako.
NGUVU YA ULINZI KATIKA
CHAKULA.
Sayansi mlo (nutritional science) imeangazia zaidi katika umuhim wa chakula kisichotengenezwa viwandani (whole food) :
kutoka hapo tunaelewa kuwa
virutubisho vilivyomo ndani ya chakula vinafanya kazi kwa ushirikiano ili
kuboresha afya zetu— ambapo vyakula vya kusindikwa (processed food) vinapoteza
kiasi kikubwa cha virutubisho, na vinaweza kusababisha magonjwa.
Tujue kuwa vitamin, amino
asidi, madini, na mafuta ya muhimu takribani 50 kwa idadi au zaidi zinahitajika
katika kila mlo tunaoupata. Na zaidi ya virutubisho-mimea
(phyto-nutrients) 1200 vinapatikana katika matunda, mbogamboga, mbegu na
vyakula vitokanavyo na wanyama.
Itaendelea….
Thursday, 1 February 2018
Tuesday, 30 January 2018
Tafakari
"Wakati mwingine ukiona watu waliokuwa karibu nawe hawako karibu nawe tena usihangaike, ujue hauna jambo jipya ni muhimu kufanywa upya kila siku ili uwe wa faida na Mungu atukuzwe kupitia wewe. Nao watakufuata”
Dr. James Makala.
0763 832798
© truth about success
Monday, 29 January 2018
KWA NINI HATUONI MAMBO MAPYA KATIKA MAISHA YETU?
Bwana yesu asifiwe ninamshukuru Mungu atupaye
kushinda na zaidi ya kushinda kila siku. Kuna vitu vichache ambavyo ningependa
kukushirikisha kwa sikuya leo.
KWANINI HATUONI MAMBO MAPYA KATIKA MAISHA
YETU.
Tukisoma
neno la Mungu tunagundua kuwa kuna mambo mema ambayo Mungu anatuwazia na
anatuahidi katika maisha yetu kila siku.
Kwa mfano tukiangalia
hapa maneno haya hapa chini…
Yer. 33:3 “ Niite, nami nitakuitikia, na kukuonyesha
mambo makubwa, magumu usiyoyajua”
Yer. 32: 26-27 “ Ndipo neno la Bwana
likamjia Yeremia, kusema, tazama, mimi ni Bwana, Mungu wa wote wenye mwili; je!
Kuna neno gumu lolote nisiloliweza?
Kumb. 4:7 “ Kwa maana liko taifa gani
, lililo na Mungu aliye karibu nao kama Bwana, Mungu wetu, alivyo, kila tumwitapo”
1 Sam. 7:23 “ Tena ni taifa lipi
duniani lililo kama watu wako, kama Israel, ambalo Mungu alikwenda kuwakomboa
kwqaajili yake, wawe watu wake mwenyewe,
akajifanyie jina, na kutenda mambo makuu kwaajili yenu, na mambo ya
kuogofya kwaajili ya nchi yako, mbele ya watu wako, uliowakomboa kutoka Misri
wawe wako, kutoka katika mataifa na miungu yao.”
Haya ni
maneno ya Mungu ambayo anayotuambia sisi, ni maneno yanayotutamkia kwenda mbele
na kuinuliwa, lakini sasa kwa nini hatuoni mambo mapya wakati ameahidi
kutuonyesha mambo makubwa na magumu tusiyo yajua?
Kumbuka kwamba
yeye Mungu/Kristo anatuambia kupitia neno lake kuwa tuombe bila kukoma (1Thes 5:17), kwa nini
alituambia kuomba kama alijua hatakuwa na muda wa kujibu hayo tunayomuomba?
Lakini pia
siyo tu alitugiza kuomba lakini pia aliahidi kujibu maombi yetu kimetokea nini
leo hatuoni hayo aliyo ahidi?
Roho Mtakatifu
aliyenipa kuandaa somo hili japo kwa ufupi ndiye atakaye tupa majibu ya nini
kilichotokea/kinachotokea hata hatuoni mambo mapya katika maisha yetu. Angalia
ahadi ya Mungu katika Biblia juu ya kuomba na ahadi yake ya kujibu maombi yetu. Kabla ya kuangalia mungu
alivyoagiza tuombe na ahadi yake ya kujibu maombi hebu kwa kifupi tujifunze
nini maana ya maombi/ kuomba.
Mt. 6:7-8;
32 “ Basi msifanane na hao; maana baba yenu anajua mnayohitaji kabla ninyi
hamjamwomba” 32 “ Kwa maana hayo yote mataifa huyatafuta; kwa sababu baba yenu
wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote”
MUNGU ALIAGIZA TUOMBE NA ALIAHIDI
KUJIBU MAOMBI YETU
Mwa. 18:17 “
Bwana akanena, je! Nimfiche Ibrahimu jambo nilifanyalo”
Zab. 25:14 “
Siri ya Bwana iko kwao wamchao, naye atawajulisha agano lake”
Amo.3:7 “
Hakika Bwana Mungu hatafanya neno lolote, bila kuwafunulia watumishi ake mabii
siri yake”
Kum. 4:7 “
Kwa maana liko Taifa gani kubwa lililo
na Mungu aliye karibu nao, kama Bwana, Mungu wetu, alivyo, kila tumwitapo”
Zab. 50:15 “
Ukaniite siku ya mateso; nitakuokoa na wewe utanitukuza”
Yer. 29:12
“ Nanyi mtaniita, mtakwenda na kuniomba,
nami nitawasikiliza”
Mdo. 2:21
“ Na itakuwa kila atakayeliitia jina la
Bwana ataokolewa”
KUNA SABABU ZA KUTOONA MAMBO MAPYA
KATIKA UKRISTO
1. KUOMBA VIBAYA
yak. 4:3 “ Hata mwaomba, wala
hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tama zenu.
” Soma vizuri hapo kuna mtumishi aliniomba nimfundishe kupiga kinanda
akasema “kaka namwomba Mungu nikijua kina Fulani watanikoma” nikamwambia hapana
huwezi kufanikiwa hivyo…lakini akawa anarudia kauli ile ile kwa akijua wata…..
basi mpaka leo ni mwezi wanne nimemfundisha hadi chord za wapi kuleee….lakini
hajapata kujua hata wimbo wa kuabudu mrahisi hawezi…wiki iliyopita alikubali
nikamwambia utubu sasa na ubadilishe kauli kuwa utajifunza kwa utukufu wa
Mungu…nimemuona leo anaendelea vizuri sana anasema anafanya kwa utukufu wa
Mungu sasa…nimetoa mfano hai ili uone wakati gani walokole tunakosea uwasaidie
na wanaokuzunguka. Anaglia hapa chini….
-yak. 4:15 “Badala ya kusema, Bwana akipenda, tutakuwa hai na kufanya hivi au hivi”
1Yn. 5: 14-15 “ Na huu ndio ujasiri tulionao kwake, ya kuwa , tukiomba
kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia. Na kama tukijua kwamba atusikia,
tuombacho chochote, twajua ya kwamba tunazo zile haja tulizo mwomba”
Mt. 26:39, 41, 44 “ Akaendelea mbele kidogo, akaanguka kifulifuli,
akaomba, akisema, Baba yangu, ikiwezekana, kikombe hiki kiniepuke; wala si kama
nitakavyo mimi, bali kama utakavyo wewe. 41 Kesheni, mwombe, msije mkaingia
majaribuni; Roho I radhi lakini mwili ni dhaifu. 44 akawaacha tena, akaenda,
akaomba mara tatu, akisema maneno yaleyale”
Tuanza kuomba vizuri
2. KUTOOMBA KWA BIDII
Suala la kuomba wote tunafahamu sana lakini shida inatokea pale
tunapokata tamaa angalia mfano huu
Lk. 11:5-10 “Akawaambia, ni nani kwenu aliye na rafiki, akamwendea usiku
wa manane, na kumwambia, rafiki yangu, nikopeshe mikate mitatu, kwa sababu
rafiki yangu amefika kwangu amefika kwangu, atoka safarini, name sina kitu cha
kuweka mbele yake; na Yule wa ndani amjibu akisema usinitaabishe mlango
umekwisha fungwa, nasi tumelala kitandani mimi na watoto wangu; siwezi kuondoka
nikupe? Nawaambia ya kwamba, ijapokuwa haondoki ampe kwa kuwa ni rafiki yake,
lakini kwa vile asivyoacha kumwomba, ataondoka na kumpa kadri ya haja yake.
Yesu alitoa mfano wa mtu asiyekata tamaa kugonga mlango.. tujifunze
kuomba hadi jambo litokee au hadi roho mtakatifu akuambie yatosha…
Angalia pia hapa….
Lk.18:1 “ Akawaambia mfano, ya
kwamba imewapasa kumwomba Mungu siku zote wala wasikate tamaa”
Kum. 4:29 “ Lakini huko kama mkimtafuta, Bwana, Mungu wako utampata,
ukimtafuta kwa moyo wako wote na roho yako yote”
Nadhani umeona kwa bidi inahitajika kw asana tu
3. KUTOOMBA KWA IMANI
Mimi sina maelezo mengi
sana lakini naomba usikie neno linasema
ebr.11:1 “ Basi imani ni
kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana”
Ebr. 11:6 “ Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza;
kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa
thawabu wale wamtafutao”
Yak. 1:6-7 “ Ila na aombe kwa
imani, pasipo shaka yoyote; maana mwenye shaka ni kama wimbi la bahari,
lililochukuliwa na upepo, na kupeperushwa huku na huku. Maana mtu kama Yule
asidhani ya kuwa atapokea kitu kwa Bwana”
Mr. 11:24 “ kwa sababu hiyo nawaambia, yoyote myaombayo mkisali, aminini
ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu”
Mt. 7: 7-11 “ Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni,
nanyi mtafunguliwa;kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye
abishaye atafunguliwa. Au kuna mtu yupi kwenu, ambaye, mwanawe akimwomba mkate,
atampa jiwe? Au akiomba samaki atampa nyoka? Basi ikiwa ninyi, mlio waovu,
mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Si zaidi sana baba yenu aliye
mbinguni atawapa mema wao wamwombao?”
Yoh. 14:13 “ Nanyi mkiomba lolote kwa jina langu, hilo nitalifanya ili
baba yangu atukuzwe ndani ya mwana”
Yon. 16:23 “ Tena siku ile hamtaniuliza neno lolote. Amini, amini,
nawaambia,mkimwomba baba neno lolote kwa jina langu atawapa”
4. DHAMBI.
Isa. 59:1-2 “ Tazama, mkono wa BWANA haukupunguka, hata usiweze kuokoa;
wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia; lakini maovu yenu
yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone
hata hataki kusikia”
hapa sitazungumza sana kwa habari ya kuokoka. Kwa ufupi tu maana ya
kuokoka ni kuachana na dhambi simamia vizuri kabisa wokovu Paulo anasema ni
kupiga vile vita vizuri vya Imani 1tim 1:18
pamoja na kuokoka kuna dhambi ambazo bado watu wameshikilia na wanasema
ni vidhambi vidogo vidogo, kama wivu mbaya wa kuona ukimsaidia mwenzio
atakuzidi, hasira, masengenyo, chuki, viuongo uongo ..eti uko mtaa wa Tanzania
unaulizwa kwenye simu uko wapi? unasema niko Kenya… acha uongo huo. kumbuka kuwa pale
ulipo kuna watu wanakuangalia wewe kama barua ya kusomwa na wao (2Kor 3:2)…. Nuru yetu na
iangaze mbele ya watu wayaone matendo yetu mema. Mat 5:16
basi kwa maneno haya mbarikiwe sana nimepewa kusema hivyo kwa uchache.
Mungu akubariki unapoendelea kuyatekeleza haya…”ukiona watu waliokuwa karibu nawe wanajitenga nawe ujue hauna jambo
jipya ni muhimu kufanywa upya kila siku ili Mungu atukuzwe kupitia wewe.”
katika haya naamini kabisa kwamba lipo jambo la kukusaidia kusogea hatua Zaidi
mbele…
Mungu akubariki sana
Dr. James Makala.
0763 832798
© truth about success
Monday, 22 January 2018
HAKI NA UPENDO.
Bwana Yesu asifiwe watumishi wa Bwana wa majeshi,
tunamshukuru Mungu atupaye kushinda na zaidi ya kushinda. Ni wakati mwing ine
tena tushirikishane maneno ya Mungu. Kadri tunavyoendelea kujifunza na
kumtukuza Mungu wetu aliye hai, tuangalie kitu hiki kinachofanya tuendelee
kuwepo hapa DUNIANI.
Kichwa cha somo kinaitwa HAKI NA UPENDO.
kwa kuanza tusome ZABURI 133 neno linasema
kwa kuanza tusome ZABURI 133 neno linasema
"1.Tazama jinsi ilivyo vyema na kupendeza, ndugu wakae pamoja
kwa umoja.
2. Ni kama mafuta mazuri kichwani, yashukayo ndevuni, ndevu za
Haruni . yashuikayo mpaka upindo wa mavazi yake.
3.Kama umande wa Hermoni ushukao mlimani pa sayuni. Maana
ndiko bwana alipoamuru Baraka, naam hata uzima wa milele."
Hebu tuangalie kidogo maana ya maneno haya mawili;
VYEMA & KUPENDEZA.
Maana ya neno VYEMA
Neno hili linatokana na neno vema
maana yake ni
jambo/kitu sahihi,kilicho haki, kilicho sawa, inavyopaswa kuwa nk.
Maana neno PENDEZA…
Neno hili lina neno penda ndani yake..wanaokumbuka Kiswahili
katika vitenzi kuna vitenzi vinaitwa vitenzi nomino yaani ni kitendo
ambacho asili yake kimetokana na jina kama kupenda kunatokana na neno upendo,
sasa kutokana na neno PENDA hiki ni kitendo lakini kikiongezwa kiambishi tamati –ez- kitalifanya neno liwe katika hali ya kutendesha… kwa hiyo PENDEZA ni kitenzi kitendeshi.
Kwa maelezo hayo
pendeza ni kitendo cha kusababisha upendo juu ya kitu Fulani. Kwa mfano
ukiona mtu amependeza ina maana kwamba kuna jambo alimefanya linalosababaisha
umpende au ukipende ndio maana mtu hukazia “yaani nguo/viatu/gari/ bustani..nk imependeza kweli nimeipenda”
Popote panapopendeza kuna Upendo…
Sasa basi wale tuliobahatika kusoma chekechea si tunakumbuka siku tulikuwa tukipata vema maswali yote, tulikuwa tunafanyiwa kasherehe ka kupewa pipi, ubuyu, dengu vibalagala n.k...ni kwa sababu tulikuwa tumefanya jambo jema ..na jambo hilo lilipendeza na kuwafanya watu watupende lakini sio kutupenda tu hata watupatie zawadi nk. Na ndipo tulikuwa tunafurahia sana ule ushindi tulioupata katika yale tuyafanyayo. Kama baba alivyofanya asubuhi ni kwa sababu kulikuwa na kuna jambo jema likampendeza mpaka akasukumwa kutoa zawadi..
Kumbe kufanya jambo lililo vyema/ haki kunaleta kupendeza/upendo.
Kwa hiyo nikimsikia Muheshimiwa Mfalme DAUDI anasema VYEMA
NA KUPENDEZA ninapata maana kuwa anasema
HAKI NA
UPENDO. Sasa kumbuka ukiona neno utakapoona mahali pameandikwa
VYEMA=HAKI au
KUPENDEZA = UPENDO.
Bila shaka utakubaliana nami kwa ufafanuzi wa utangulizi
niliotoa.
Tuangalie kwenye vipengele vichache vifuatavyo kabla niende
kukesha hukoo kanisani…
a.
Muanzilishi wa haki na upendo.
b.
Umuhimu/ ulazima wa Haki na upendo.
c.
Faida za haki na upendo.
d.
Hasara za kutokutenda haki na upendo.
A.
MUANZILISHI WA HAKI NA UPENDO .
Mungu ndiye muhasisi au muweka jiwe la
msingi la haki na upendo maana yeye ndiye HAKI NA UPENDO fuatilia hapa…
1.HAKI
i. Mungu ndiye mmiliki wa haki
Isaya
45:21…ni nani aliyeyahubiri hapo zamani? Si mimi, Bwana? Wala hapana
Mungu zaidi ya mimi, Mungu mwenye haki, mwokozi; hapana mwingine zaidi ya mimi.
Utaona anaitwa MUNGU WA HAKI., zaburi 4;1
Kwa maana , wakiwa hawaijui haki ya Mungu
na wakitaka kuithibitisha haki yao wenyewe , hawakujitia chini ya HAKI YA
MUNGU…Rum 10;3
ii. Mungu ndiye awezaye kuwahesabia haki
watu.
tukihesabiwa haki na MUNGU tuko salama
maana yeye ndiye mmiliki wa haki hakuna awezaye kutushitaki…..…ni nani
atakayewashitaki wateule wa Mungu? Mungu ndiye mwenye kuwahesabia haki..8:33
2. UPENDO.
i. Mungu mwenyewe ni upendo.
Yeye asiyependa hakumjua Mungu maana Mungu
ni Upendo…1 yoh 4:8.
Sikia hapa MUNGU =UPENDO
Yaani mtu ambaye hajaokoka akikuambia anakupenda,
ujue anakudanganya ni kwamba amekutamani
tu, ambao hawajaokoka hawajui kupenda maana MUNGU ambaye ni UPENDO
hayumo ndani yao……nasi tumelifahamu pendo
alilonalo Mungu kwetu sisi na kuliamini. Mungu nu upendo, naye akaaye katika
pendo hukaa ndani ya Mungu, na Mungu ndani yake. so be Eyes everyone.
B.
UMUHIMU AU ULAZIMA WA HAKI NA UPENDO.
1.
NI AMRI KUU YA MUNGU.
Marko 12:30-31
Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote na kwa
akili zako zote na kwa nguvu zako zote… na ya pili ndio hii, mpende jirani yako
kama nafsi yako. “HAKUNA AMRI ILIYO KUU KULIKO HIZI”
YESU alikuwa smartmind sana, maana wayahudi walikuwa wanajifanya wanajua
sana amri za Mungu na maandiko lkn walikuwa hawayaishi yale waliyoyameza.… kwa
hiyo Yesu aliwaambia kuwa wanapotea kwa sababu hawajui uweza wa Mungu uliomo
katika neno la Mungu… sasa kurahisisha akafanya summary ya amri zote 10 zikawa
2 tu. Kwa kisukuma wanasema 10 in 2.
2.
UPENDO NA HAKI HUAMBATANA
Kama tulivyoona hapo juu lengo kubwa la amri za Mungu ambazo zimefichwa
ndani ya UPENDO dhamira yake ni kuleta HAKI ndio maana somo linaitwa HAKI NA
UPENDO . maana PALIPO NA HAKI KUNA UPENDO PALIPO NA UPENDO KUNA HAKI.
Zaburi
133.
3.
PASIPOKUWA NA UPENDO HAIWEZAKANI KUMPENDEZA
MUNGU.
Nijaposema kwa lugha zote za wanadamu na za malaika kama sina upendo,
nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao…
Kichwa cha habari chajieleza. Nasi twajua mungu baba, mungu mwana naye
roho mtakatifu wako katika hali ya upendo ndio maana hakuna kitendeacho kazi
pasipo kujulikana kwa sehemu zingine..
itaendelea....
Mbarikiwe sana.
Dr. James
Subscribe to:
Posts (Atom)
-
Bwana yesu asifiwe ninamshukuru Mungu atupaye kushinda na zaidi ya kushinda kila siku. Kuna vitu vichache ambavyo ningependa kukushirikish...
-
TAMBUA KUSUDI LA WEWE KUWEPO HAPA DUNIANI "Janga kubwa katika maisha sio kifo bali ni maisha bila kusudi" Dr. M...
-
TYPHOID FEVER/homa ya matumbo Habari za leo ndugu msomaji wa blog ya KUSUDI LAKO. Karibuni katika somo la leo ambapo tunazungumzia ugonjw...